Zilizopendwa Zaidi

Wapendwa
Breaking
Inapakia...

AJALI ILIYOUA 35, NDEGE AINA YA DC 8 YAPATIKANA KUPELEKA MAJERUHI MAREKANI KWA MATIBABU ZAIDI

Nikiwa na Dkt. Urio, Mkuu wa Hospitali ya Mt Meru, na mtoto Doreen Mshana tulipomtembelea alasiri leo kumwona yeye pamoja na watoto wenzake wawili wanaoondelea na matibabu kutokana na ajali ya Karatu. Wazazi (akina Mama) wote watatu wa watoto hawa wanaelekea Dar es Salaam jioni ya leo kwa maandalizi ya kupata hati ya kusafiria na baadae kuomba visas kwa ajili ya kuwasindikiza watoto wao kwenye matibabu zaidi Nje ya nchi kama alivyoeleza Mh Makamu wa Rais wakati wa kuwaaga wenzao waliotangulia kutokana na mkasa wa ajali hiyo. Tuendelee kuwaombea Mungu aifanikishe safari hiyo kwa utukufu wake mwenyewe. Iwe heri na salama kwao! tmp_30576-FB_IMG_1494526536680-1667873048.jpg
=======UPDATES.
Tumefanikiwa kupata ndege aina ya DC 8 kutoka Shirika la Samaritan Purse linaongozwa na mtoto wa Billy Grahm, aitwaye Franklin Grahm kwa ajili ya kuwasafirisha watoto Doreen, Sadia, na Wilson pamoja na wazazi wao watatu (Mama zao), ikiwa ni pamoja na Muuguzi Simphorosa Silalye, na Daktari Elias Mashalla wa Mt Meru hospitali. Ndege hii inaondoka jioni ya leo kutoka mji Mkuu Charlotte, Jimbo la North Carolina nchini Marekani na inatarajiwa kuwasili uwanja wa ndege wa Kilimanjaro majira ya jioni, Jumamosi, Mei 13. Endapo upatikanaji wa visas utafanikiwa hapo kesho kama tunavyo tarajia, wasafiri wataondoka asubuhi ya Jumapili, Mei 14 kuelekea Amerika. Ndege hii aina ya DC 8 itatarajiwa kutua Mjini Charlotte, NC, na wagonjwa pamoja na waliowasindikiza wataingia katika ndege nyingine maalumu ya kubeba wagonjwa (Air Ambulance) hadi mji wa Sioux City, Iowa ambako watapokelewa na Uongozi wa Hospitali na Mercy na Shirika la STEMM.

 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 maoni :

Chapisha Maoni