Zilizopendwa Zaidi

Wapendwa
Breaking
Inapakia...

BABA WA TAIFA ASEMA "WOTE MAZIGANYANJA" IJUE LIST YA WALIOSHIRIKI MGAWO WA ESCROW

MTANZANIA lilimpomtafuta Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP), Biswalo Mganga kupata ufafanuzi wa kina wa hatua ya ofisi yake kushikilia mali za Sethi na Rugemalira, hakupatikana na alipopigiwa simu hakupokea.

Mbali na hayo imeelezwa kuwa orodha ya waliopata mgawo wa fedha hizo za Escrow imezidi kuongezeka, wakiwamo vigogo kutoka wizara nyeti, taasisi, viongozi wa dini na mashirika yasiyo ya kiserikali na tayari baadhi yao wameanza kuhojiwa na Takukuru mapema wiki hii.

Image result for andrew chenge, anna tibaijuka, william ngeleja imagesAndrew Chenge,William Ngeleja,Anna Tibaijuka

Taarifa za ndani zinaeleza kuwa idadi ya waliohojiwa imefika zaidi ya watu 30 hadi sasa.

Miongoni mwa wanaotajwa kuhojiwa na Takukuru wamo baadhi ya mawaziri wa Serikali ya Awamu ya Nne na mtoto wa kigogo wa Serikali, ambao inaelezwa kuwa huenda wakafikishwa mahakamani Jumatatu, huku wengine wakiendelea kuhojiwa zaidi.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 maoni :

Chapisha Maoni