Zilizopendwa Zaidi

Wapendwa
Breaking
Inapakia...

HUREE!!! MAN U YATINGA FAINALI, Ilikuwaje? endelea.......

Manchester United yatinga fainali ya kombe la Europa

United itacheza dhidi ya Ajax Amsterdam ya Uholanzi ambayo ilifuzu kwa kuishinda Lyon ya Ufaransa.
Ikiwa kifua mbele kwa 1-0 ugenini United ilipata bao lao kupitia Marouane Fellaini aliyefunga kwa kichwa kufuatia krosi ya Marcus Rashford.
Lakini Celta Vigo iliohitaji mabao mawili ili kufuzu ilisawazisha kupitia Facundo Roncaglia na kuifanya nusu fainali hiyo kuwa na tumbo joto.
Mlinzi wa United Eric Baily na Roncaglia walipewa kadi nyekundu baada ya kuzua ghasia uwanjani huku Man United ikilinda ushindi huo na kufuzu fainali.
Hatahivyo walisheherekea baada mshambuliaji wa Celta Vigo John Guidetti kukosa fursa nzuri ya kupata ushindi wa kuwaweka mbele wageni hao katika kipindi cha lala salama.
Jumla hiyo imesaidia Manchester United kufuzu katika fainali na hatua nzuri ya kufuzu katika kombe la vilabu bingwa Ulaya .
Watakutana na Ajax ambao waliwashinda Lyon katika nusu fainali nyengine katika mji wa Stockholm mnamo mwezi Mei 24.

Chanzo: BBC SWAHILI
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 maoni :

Chapisha Maoni