Zilizopendwa Zaidi

Wapendwa
Breaking
Inapakia...

SOMA HIKI KISA CHA KWELI, KAFIKRI FOOLS DAY KAKUTA KWELI, BUT LATE JAPO!

Siyo kila taarifa ya dharura unayoelezwa siku ya wajinga ukaipuuzia zingine za kweli, kwani matukio hayo hayawezi kutokea hiyo tarehe?, tafakari na fuatilia kisa hiki cha kweli kilichomtokea huyu brother,


Ni miaka kadhaa imepita lakini Jamani siku kama ya Leo sitaisahau,nilikuwa nipo hostel mwaka wangu wa mwisho wa masomo chuo fulani hapa dar,nilikuwa najiandaa kwenda darasani,nakumbuka nilipigiwa simu na rafiki wa mpenzi wangu akaniambia babe wangu yupo eneo la lakini kazimia amepoteza fahamu nikacheka saana nikakata simu.
Baadae Dada ake akanipigia akaniambia umesikia doctor anaumwa nkamwambia Leo siku ya wajinga WiFi,akagutuka akasonya akasema pumbavu zao,akakata simu.

Nikaingia zangu darasani. Baadae mdogo wake akanipigia ambae anasoma maeneo ya muhimbili hapohapo akaniambia hivyo hivyo jamaa anaumwa nikamwambia Leo siku ya wajinga buana.

Akasema yaani nilishafka Hadi nje hapa ya jengo la emergence,ngoja nirudi alionekana kumind kiasi Fulani,sasa ile anageuka pale emergence wanataratibu za kutangaza majina ya wagonjwa kwa ajili ya ndugu zake waingie ndani. Si ndio akasikia ndugu wa doctor Fulani Fulani.

Akasema wameniona nipo hapa ndio wananiita. Akasepa,lakini akafika sehemu kabla hajatoka eneo la muhimbili akakutana na mfanyakazi mwenzie wa department moja akauliza ndio unatoka kumchek kaka yako anaendeleaje?

Akauliza vizuri,ndio akastuka kumbe kweli,ikabidi anitext Shem ni kweli anaumwa yuko emergence ndio naenda kumuona. Nikamuulza umejuaje?Una uhakika hauchezewi akili? Akaniambia Fulani kaniuliza hivi. Duh!!nilipagawa halafu nikachukia ujinga wa hii siku.

Ikanibidi nitoke darasani nianze safari to Muhimbili yaani namkuta unconscious kweli..duh!!nikijikuta nalia tu,nikafeel guilty kwa kuwaambia watu cha lipuuzi April fool wakati mtu yupo serious sick.

Kama dakika kumi nimesimama pale pale pembeni ya kitanda machozi yananitoka,nikaona mtu ananishika mkono Ndio akawa anarudiwa na fahamu ananiuliza mbona unalia.

Ikabidi nitoke niwapigie ndugu zake wengne niwape taarifa. Sitaisahau hii siku na ujinga wake,ambao watu tunaweza kufanya jambo lenye madhara makubwa kwa ajili ya hii siku. 


Source: Jamii Forum
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 maoni :

Chapisha Maoni