Jana mahakamani alikuwa akilalamika kwamba kwanini ashitakiwe peke yake?
Baadhi ya watu waliuliza, alipoenda kuharibu shamba la Mbowe alienda na nani?
Alimshirikisha Mkuu wa Mkoa au Mwanasheria wa Serikali?
"Mnapenda sana sifa, ngoja muone matokeo ya Kukurupuka". alisema mwananchi mmoja
aliendelea kusema "Mimi nlimuona Mkuu wa Wilaya kwenye picha akiharibu shamba la Mbowe tena aling'oa huku amesindikizwa na askari. "
"Hii iwe fundisho". alisisitiza
Mkuu wa Wilaya ya Hai, Gelasius Byakanwa ameiomba Mahakama imuunganishe Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) katika kesi ya madai ya fidia ya Sh549 milioni iliyofunguliwa na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
Kiini cha kesi hiyo ni hatua ya Byakanwa, kudaiwa kuharibu miundombinu ya umwagiliaji ya shamba (green house) la kampuni ya Kilimanjaro Veggie Ltd (KVL) linalomilikiwa na Mbowe, Juni 19.
Mbowe, ambaye ni mbunge wa Hai na mkurugenzi mwendeshaji wa KVL, amemshtaki mteule huyo wa Rais kama mtu binafsi.
Ombi la kutaka AG aunganishwe, liliwasilishwa mahakamani jana na wakili Modestus Njau anayemtetea Byakanwa mbele ya Jaji Mfawidhi wa Mahakama Kuu, Aishiel Sumari.
Hizi ni picha zinazomuonesha Mkuu wa Wilaya ya Hai Gelasius Byakanwa akiharibu shamba la Freeman Mbowe
Chanzo: Jamii Forum
0 maoni :
Chapisha Maoni