Zilizopendwa Zaidi

Wapendwa
Breaking
Inapakia...

AJALI MBAYA IMETOKEA ENEO LA UKONGA DAR, BAINA YA DALADALA AINA YA COASTER NA LORI LA MCHANGA

Kuna jamaa imenitaarifu maeneo ya Ukonga Dar e s Salam, kati Magereza na Madafu kumetokea ajali mbaya, daladala aina ya coaster imepigwa ubavuni na roli la mchanga.
Kwa mujibu wa maelezo yake kuna majeruhi wengi na watu kadhaa wanahisiwa kupoteza maisha.

Kama kuna mtu yupo maeneo hayo tunaomba afuatilie tukio hili kwa karibu zaidi na atujuze kwa uzuri zaidi.

=======

FB_IMG_1499143252446.jpg
Watu kadhaa wanahofiwa kujeruhiwa baadhi ikiwa vibaya baada ya gari walilokuwa wakisafiria (daladala) kugongana na lori la Taka eneo la Ukonga Madafu jijini Dar es Salaam.

Daladala hilo lifanyalo safari zake kati ya Gongo la Mboto na Makumbusho liligongwa ubavuni kuanzia mlangoni na kusababisha majeruhi hao huku wengine wakihofiwa kufa, wakati daladala hilo likitaka kulipita gari lingine.

Baadhi ya Mashuhuda wamesema dereva wa daladala alikuwa akijaribu kulipita lori lingine ndipo akataka kugongana na lori hilo uso kwa uso na katika harakati za kulikwepa likagongwa ubavuni na kujeruhi watu.
 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 maoni :

Chapisha Maoni