Zilizopendwa Zaidi

Wapendwa
Breaking
Inapakia...

WABUNGE WATAKA SHUGHULI ZA BUNGE ZIAHIRISHWE, ILI WAJADILI MAFURIKO

Wabunge wametaka shughuli za Bunge za leo ziliahirishwe ili wabunge wajadili tatizo la mafuriko liloyakumba maeneo mbalimbali nchini ambayo yameacha watu bila makazi na kusababisha vifo.
 Image result for mafuriko dar 2017

Wabunge hao walisimama na kuomba miongozo hiyo leo asubuhi muda mfupi baada ya kipindi cha maswali na majibu bungeni.

Walioomba miongozo ni Mbunge wa Korogwe Vijijini (CCM) Stephen Ngonyani, James Mbatia (NCCR Mageuzi) na Rashid Shangazi (Mlalo-CCM).

Ngonyani maarufu kama Majimarefu ametumia kanuni ya 68(7) alisema kuwa kuna matatizo makubwa ya mafuriko nchini.

“Haswa kwenye mkoa wangu wa Tanga, kumekuwa na maafa, leo hii tunavyoongea kuna watu 1000 hawana chakula, mahali pakuishi na hawana msaada wowote lakini itawasaidiaje hawa watu wakati kamati za afya zikiendelea na utaratibu,”amesema.

Amesema watu wanaathirika na wanaweza kufa wakati wowote.

Shangazi amesema anasimama kwa kanuni 47 (1) akitaka shughuli za Bunge ziahirishwe ili wabunge wajadili kuhusu mafuriko hayo.

“Sasa hivi katika mkoa wa Tanga kuna mafuriko makubwa sana. Na jana yametokea maporomoko katika milima ya usambara, eneo la barabara Lushoto- Arusha- Mombo, Pangani kwenda Tanga, Mombo kwenda Lushoto na Kilindi kwenda Morogoro shoto zilifungwa,”amesema Shangazi.

Chanzo:
Mwananchi
 
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 maoni :

Chapisha Maoni