Zilizopendwa Zaidi

Wapendwa
Breaking
Inapakia...

VIDEO NA VITUKO VYA MBUNGE HALIMA MDEE

Nadhan hapa tunapasa kuweka itikadi zetu za vyama ,dini na kabila pembeni. kuna kipindi tunapaswa kusimama kama watanzania tukaweka mambo mengine yote mifukoni mwetu tukabaki na utanzania. Tanzania ya sasa si tanzania ya jana...inabadilika inakuja na mambo leo ambayo mengine si mazuri. Nimemsikia mbunge mmoja akiongea lugha ya ajabu sana bungeni ambayo sitegemei mbunge msomi na ampambanaji ongee hata kama alikwazika sana. Angalau kistaarabu angeomba msamaha maana wanasema ada ya mja hunena uungwana ni vitendo. Kwa mbunge kutamka maneno "fala" "mpumbavu" si maneno mazuri ingawa sishangai hili tatizo si kwa wabunge vijana tu . tulishawah sikia mtu mzima mmoja akiitwa wenzie "wapumbavu" si maneno ya kistaarabu tukiacha ashakum si matusi. Kuna lugha za mitaani hizo zisipelekwe bungeni kwa nini wabunge huwa hawapewe semina ya communication skills? maneno kama "kimenuka" "fala", "wapumbavu" hatutegemei kuyasikia bungeni. Wapumbavu wote basi wanapotamkwa watamkwe pia na huo upumbavu walioufanya au nena wasiishiwe kuitwa wapumbavu. Nimesikitika sana kwa aina hii ya wabunge akina kibajaji lusinde, akina Halima Mdee, Sugu n.k tunategemea nini? ni wapi tulipokosea sisi watanzania? Najua bado kuna watu watakuja kutukana hapa na kumtetea.Kudhihirisha kuwa tuna taifa ambalo either limeathirika na viroba au matumizi ya bangi lakini sisi wenye akili timamu hatutanyamaza. "Acha Tu niseme Ukikasirika Basi"
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 maoni :

Chapisha Maoni