Zilizopendwa Zaidi

Wapendwa
Breaking
Inapakia...

KOMBORA LA KOREA KASKAZINI LASHINDWA KUPAA

Kombora la Korea Kaskazini lashindwa kupaa siku moja baada ya maonyesho ya zana za kijeshi,

Kombora la Korea Kaskazini lashindwa kupaa siku moja baada ya maonyesho ya zana na kijeshi
Kombora la Korea Kaskazini lashindwa kupaa siku moja baada ya maonyesho ya zana na kijeshi 

Korea Kaskazini imejaribu kufyatua kombora moja lakini likakosa kupaa angani, siku moja tu baada ya kuonya Marekani kuwa haiogopi vitisho vyake vya kivita.
Jeshi la Marekani lilisema kuwa kombora hilo lililipuka sekunde chache baada ya kufyatuliwa katika ufuo wa Mashariki wa Korea Kaskazini.
Afisa mmoja wa Marekani alisema kuna uwezekano mkubwa kuwa kombora hilo halikuwa la masafa marefu linaloweza kutoka bara moja hadi jingine.
Rais Trump alifahamishwa juu ya jaribio hilo lililofanywa masaa machache kabla ya Makamu wa Rais Mike Pence kuwasili Korea Kusini, kwa mashauri kuhusiana na Pyongyang na mipango yake ya makombora ya kinyukilia.
Hali ya uhasama kati ya Korea Kaskazini na Marekani imekuwa ikipanda, huku kila upande ukijigamba jinsi utakavyoweza kuchafua upande mwingine.
Mnamo Ijumaa Uchina iliitisha mkutano unaonuia kutuliza uhasama huo. 

Source: Jamii Forum
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 maoni :

Chapisha Maoni