Zilizopendwa Zaidi

Wapendwa
Breaking
Inapakia...

SAMSUNG KUPATA HASARA YA PAUNDI 4.4BN

Samsung kupoteza faida ya £4.4bn kutokana na Note 7

Samsung Note 7

Kampuni ya Samsung imesema gharama ya kuacha kuuza simu yake ya karibuni zaidi ya Galaxy Note 7 sitakuwa zaidi ya £4.4bn ($5.4bn).
Kampuni hiyo ya Korea Kusini tayari imepunguza matarajio yake ya faida ya robo ya tatu ya mwaka kwa £1.9bn ($2.3bn).
Mnamo Ijumaa, kampuni hiyo ilisema inatarajia kuathirika zaidi na kupoteza won 3.5 trilioni zaidi ($3bn, £2.5bn).
Samsung iliwashauri wateja waliokuwa wamenunua Note 7 warejeshe simu walizokuwa wamenunua baada ya visa vya simu hizo kulipuka na kuwaka moto kuripotiwa.
Hitilafu ilidhaniwa kuwa kwenye betri.
Kampuni hiyo hata hivyo iliacha kuunda na kutengeneza simu hizo baada ya simu mpya walizokuwa wamebadilishiwa wateja, ambazo zilidhaniwa kuwa salama, kuanza kushika moto.
Simu hiyo ilikuwa imezinduliwa Agosti ikitarajiwa kushindana na simu mpya ya Apple iPhone7.
Licha ya matatizo hayo, Samsung Electronics imesema inatarajia kupata faida ya won 5.2 trilioni (£3.7bn) robo ya tatu ya mwaka huu.
Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 maoni :

Chapisha Maoni