Zilizopendwa Zaidi

Wapendwa
Breaking
Inapakia...

KINA DADA WA ASERNAL OUT KOMBE FA


Kina dada wa Arsenal watupwa nje Kombe la FA

Marisa Ewers alijiunga na Birmingham City kutoka Bayer Leverkusen Aprili 2016
Marisa Ewers alijiunga na Birmingham City kutoka Bayer Leverkusen Aprili 2016

 

Mabingwa watetezi wa Kombe la FA la Wanawake nchini Uingereza, Kina dada wa Arsenal, wametupwa nje ya michuano ya mwaka huu.
Hii ni baada ya kuchapwa 1-0 na kina dada wa Birmingham City katika hatua ya robofainali.
Bao la Birmingham lilifungwa na Marisa Ewers dakika ya 77.
Kipa wa Birmingham Ann-Katrin Berger alifanya kazi ya ziada kuwazuia Arsenal kufunga. Aliokoa makombora kutoka kwa Kim Little, Danielle Carter na Danielle van de Donk kipindi cha kwanza.
Katie McCabe na Jordan Nobbs walishambulia lakini wakashindwa kulenga vyema wavu upande wa Arsenal muda mfupi kabla ya Ewers kufunga.
Droo ya nusufainali itafanyika baadaye Jumatatu.



Share on Google Plus

About Unknown

This is a short description in the author block about the author. You edit it by entering text in the "Biographical Info" field in the user admin panel.

0 maoni :

Chapisha Maoni