Gazeti la Mwanaspoti, limeripoti ya kuwa Mhe Zitto Kabwe kujitosa kwenye kinyang'anyiro cha urais TFF,
Naona wanasiasa, hasa wa vyama vya upinzani, wakiendelea kujiimarisha katika anga zingine mbali na siasa na safari hii mwanasiasa mwingine wa upinzani, Zitto Zuberi Kabwe nae anatajwa kujitosa kugombea urais wa Shirikisho la Mpira Nchini(TFF) kama ambavyo mwanasiasa mwenzake wa upinzani,Tundu Lissu alivyojitosa na hatimae kushinda uraisi wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika(TLS) hivi karibuni.
Habari ya Zitto kujitosa kwenye kinyang'anyiro cha uraisi wa TFF imeripotiwa katika gazeti la MwanaSport la siku ya leo.
Swali ni je,zile figisufigisu za kisiasa alizofanyiwa Lissu wakati anataka kugombea uraisi wa TLS tutaziona tena kwa Zitto?
Tusubiri.
0 maoni :
Chapisha Maoni